ASKOFU AKUTWA AMEFARIKI BAADA YA KUPOTEA SIKU TATU



Askofu mstaafu wa Kanisa la Anglikana Tanzania Dayosisi ya Victoria Nyanza (DVN), Boniphace Kwangu amekutwa amefariki dunia katika mazingira ya kutatanisha.

Marehemu alitoweka tangu Novemba 28 na mwili wake kukutwa ukielea katika Ziwa Victoria eneo la Bukumbi Wilayani Misungwi.


Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu leo Ijumaa Desemba 2, Askofu wa Kanisa la Anglikana Tanzania Dayosisi ya Victoria Nyanza (DVN), Zephania Ntunza amethibitisha kifo cha mtangulizi wake huyo ambaye mwili wake ulikutwa ukiwa umetelekezwa wilayani humo jana.



Post a Comment

Previous Post Next Post