SERIKALI KUWAKOPA SIMU WANANCHI

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema Serikali ina mpango wa kutafuta njia ili kumwezesha Mtanzania wa kawaida kumudu gharama za kununua simu janja (Smartphone) kwa kukopewa mkopo na kurejesha kidogokidogo.


Akizungumza katika uzinduzi wa mnara wa mawasiliano ya simu katika kijiji cha Kinenulo mkoani Njombe uliojengwa kupitia ruzuku inayotolewa na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote ( UCSAF ), waziri amebainisha kuwa malengo ya Serikali ni kuhakikisha kila Mtanzania anaunganishwa na huduma ya mawasiliano.


Aidha, amesema tayari wameanza mchakato kwa kufanya mazungumzo na kampuni mbalimbali za simu kwa ajili ya kufanikisha mpango huo.

 

Post a Comment

Previous Post Next Post