Mitandao hasa ya kiingereza nchi kadhaa imebeba habari ikimnukuu Hamisa Mobetto akidaiwa kusema kwamba yeye na Tanasha ni matamanio yao kuwaona pamoja watoto wao wote waliozaa na Diamond Platnumz wakiwa karibu kama ndugu lakini kikwazo kikubwa ni Zari ambaye hana taimu nao kabisa
"Mimi na Tanasha tupo vizuri, tunawasiliana sana lakini tatizo ni mwenzetu(Zari), anatudharau na pengine hiyo ndio sababu hataki hata watoto wetu wawe karibu, lakini yote ni sawa tu" amedaiwa kunukuliwa mrembo huyo wa kibao cha Madam Hero
Mobetto na Tanasha kwa nyakati kadhaa washaonekana pamoja ikiwemo kushirikiana kikazi
Post a Comment